A. Jina la idara
Idara hii inaitwa idara ya
Uinjilisti na Umisheni.
B.
Maono ya idara (vission)
Kutoa fursa kwa watu wote walioko
ndani na nje ya jimbo la Mbeya kusikia Injili ya Yesu kristo, kwa kuanzisha
mtembeo wa upandaji wa makanisa yatakayojizidisha katika kila jamii iliyopo
duniani kupitia nyenzo ya uinjilisiti.
C.
Dira ya idara. (Mission)
Kuhubiri Injili na kupanda makanisa yenye kujizidisha.
Tunaamini kwamba Injili itahubiriwa kwa haraka
pindi tutakapofaulu kuwafanya waamini kuwa wanafunzi na kama kanuni ya
mazidisho itafanya kazi;
“kila mmoja kufundisha
mwingine”
Na mambo yale uliyoyasikia
kwangu mbele ya mashahidi wengi hayo uwakabidhi watu waaminifu wataka faa
kuwafundisha na wengine. (2Tim 2:2)i
Tukifanya ki-Biblia tunapata
matokeo ya kiBiblia.
Dira ya idara hii ni kuhakiskisha
kila mwammini wa kanisa la mahali pamoja anajihusisha kikamilifu na agizo
kuu. Kuhamasisha na kutia moyo waaamini kutumbua kwamba agizo kuu linamhusu
kila mmoja yeye binafsi na kanisa kwa ujumla.
D. Kauli lengo
Wakati wa Mavuno ni Sasa.
E.
Andiko
la idara
Yohana 4:35
,,
“Inueni macho yenu myatazame mashamba yakuwa yameshakuwa meupe tayari kwa mavuno”
F. Malengo ya Idara
Malengo ya idara yamegawanyika
katika maeneo mawili ambayo ni
·
Malengo ya jumla (general objecive)
Malengo ya jumla yanaelezea
kusudi hasa la kuwepo kwa idara hii na kile kinachpaswa kutekeleza kwa ujumla
wake.
·
Malengo mahususi(Spesific objective)
Malengo mahususi yanafafanua
malengo ya jumla kwa kuainisha mambo maalumu ambayo ni msingi wa uwepo wa idara
hii. Malengo mahususi yanatuwezesha kupata matokeo ya muda mfupi na yenye
kupimika .
§
Malengo
ya jumla
Idara hii ya uinjilisti na
umisheni imeanzishwa kwa kusudi la kuharakisha utekelezaji wa Agizo kuu la
Bwana wetu Yesu Kristo.
Akawaambia “Enendeni ulimwenguni
mwote mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe” Marko 16:14
Maelezo haya ni amri ambayo iko
wazi na inadai utekelezaji. Hivyo idara hii iko kwa kusudi hili la
kuhubiri Injili kwa watu wote na kupanda makansa katika maeneo mbalimbali, ndani
na nje ya jimbo la Mbeya.
Tunaamini kwamba
uinjilisti na umisheni ndio kipaumbele cha kwanza cha Kanisa . Wosia wa
mwisho wa Yesu Kristo kwa wanafunzi wake ulihusu Agizo kuu yaani Uinjilisti na
umisheni. Matendo ya Mitume1:8
Wosia wa mwisho wa mtu huwa
unashikwa na kufanyiwa kazi kuliko kitu kingine chochote kile. Hivyo kanisa
linatakiwa kuupa uzito wa kipekee wosia huu wa Agizo kuu.
Idara hii inalenga kuhamisisha na kutumia rasilimali mbalimbali za kikanisa kuanzia ngazi ya tawi, parishi na jimbo
katika kuhubiri Injili na kupanda makanisa yenye kujizidisha. Tunaamini
raslimali kuu ni watu hivyo wamini wanatakiwa kufanywa wanafunzi wenye
uwezo wa kujizidisha ili kuufikia ulimwengu wote kwa Injili. Kuhakikisha watu
wote wanafikiwa pale walipo kwa Injili ya Yesu Kristo.
Malengo mahususi
1.
Kuanzisha idara ya uinjilisi na umisheni kuanzia
tawini hadi parishi.
2.
Kuandaa makongamano ya wahubiri na waimbaji ili
kupeana uzoefu na changamoto katika huduma ili kuweza kuboresha huduma za
waimbaji na wainjilisti walioko ndani ya KLPT jimbo la Mbeya.
3.
Kuanzisha mfuko wa jimbo wa huduma ya Uinjilisti na umisheni.
·
Kupendekeza asilimia tano (5%) ya mapato ya kila
kanisa kuingia katika mfuko wa uinjilisti na umisheni.
·
Kuendesha halambee kwaajili ya kukuza mfuko wa
Injili.
·
Kuanzisha miradi mbalimbali mfano shule,
gazeti, redio Nk
4. Kuanzisha mtandao wa
maombi wa uinjilisti na Umisheni.
5. Kufanya uinjilisti wa
Maandiko
Kuandaa vipeperushi, majarida na
vitini kwaajili ya uinjilisti wa maandiko.
6. Kufanya Uinjilisti kupitia
vyombo vya habari, mfano Redio, magazeti na luninga.
7. Kuanzisha tovuti ya idara
Kuanzisha tovuti ya idara ambayo
itatumika kufaya uinjilisti kupitia mtandao.
Kufanya uinjilisti kupitia
mitandao mbalimbali ya kijamii
8. Kukuza afya ya kanisa.
Kuhakikisha makanisa yote
ya KLPT Jimbo la Mbeya yanakuwa na vichocheo mbalimbali
vitakavyosababisha kukua kwa vipawa, karama na huduma za waamini wote na
kuwafanya wanafunzi weye kujizidisha ili kuleta matokeo makubwa sasa katika
uvunaji, kwa kufanya yafuatayo .
·
Kila kanisa la mahali pamoja(tawi na parishi)
kuanzisha ibada za maombi na maombezi ya nguvu kama chambo cha uvunaji.
·
Kuboresha mifumo ya ibada. Ibada zisikae
kiburudani zaidi. Ibada zisigeuke kuwa ukumbi. Mambo ya kiroho yapewe kipaumbele
zaidi katika ibada.
·
Uboreshaji wa majego na upatikanaji wa vyombo
vya mziki na injili.
G. Malengo ya idara kwa mwaka wa 2015
Idara hii imeweka mipango
mikakati inayotakiwa kutekelezwa ndani ya mwaka wa 2015 kama ifuatavyo.
Kuanzisha idara ya uinjilisti
mataiwini na parishi zote.
Utekekelezaji wake.
Viongozi wa idara hii
watashirikiana na wachungaji wa makanisa husika katika kuanzisha idara ya
Uinjilisti na Umisheni makanisani.
Utekelezaji wake ni kuanzia
mwezi wa kwanza 2015 hadi mwezi wa tano 2015.
Kupanda makanisa mawili.
Kuandaa mikutano ya Injili miwili
kuhubiri na kupanda kanisa katika vijiji/mitaa miwili katika jimbo la
Mbeya.
Utekelezaji ni Kuanzia mwezi wa sita
hadi mwezi wa kumi na mbili 2015.
Kuanzisha tovuti ya Idara ya Uinjilisti
na Umisheni.
Kufanya uinjilisti kupitia mitandao ya kijamii, kama vile
facebook, twiter n.k
Utekelezaji wake ni mwezi
Januari 2015 na kuendelea.
Kuanzisha vipindi vya uinjilisti
redioni.
Kuhakikisha angalau kwa mwezi
tunakuwa na kipindi redioni.
Utekelezaji wake ni kuanzia
mwezi wa tano na kuendelea.
Kuanzisha mfuko wa idara ya
uinjilisti na Umisheni.
Kufungua akaunti , benki kwaajili ya kutunza fedha za idara.
Utekelezaji wake ni mwezi Julai
hadi Agosti 2015.
H. Changamoto.
Idara hii ni mpya na imeanzishwa
bila kuwepo maandalizi ya kutosha kwani inawawia vigumu viongozi wa idara
kuongoza idara bila kuwepo mwongozo au maelekezo yenye kutoa mwanga wa
uendeshaji wa idara.
Hivyo viongozi wanajikuta
wanalazimika kuendesha idara kwa mfumo wanaouona wao unafaa. Idara imeanzishwa
lakini hakuna muunganiko kati ya matawi, parishi, jimbo na taifa.
Tunaamini waanzilishi wa idara
ndio wenye dira na maono ya idara hii. Hivyo kupewa
kuongoza idara bila kupewa mwongozo ni kupewa kazi ya kuanzisha msingi juu ya
msingi, jambo ambalo haliwezekani kiBiblia.
I. Mapendekezo
Mapendekezo yetu kwa kamati
tendaji ya jimbo na taifa kwa ujumla ni kwamba iandae mwongozo wa idara hii ili
kuturahisishia utendajikazi.
Pia mfumo wa uongozi uboreshwe kwa kuainisha viongozi kimadaraka na majukumu yao yaainishwe wazi kila mmoja.
Tunapendekeza mwongozo huo
utakaoandaliwa uhusishe vitu vifuatavyo
·
Jina la idara
·
Malengo/makusudi ya idara
·
Nembo ya idara
·
Maono ya idara
·
Dira ya
idara
·
Muundo wa uongozi.
·
Sifa za viongozi
·
Majukumu ya uongozi kila mmoja
·
Muda wa kushika uongozi
·
Vikao vya uongozi
·
Vyanzo ya
fedha vya kudumu.
Kwa msaada wa Mungu
tutatenda makuu,….. Zaburi
60:12
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni